Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 16, 2014

Siddiqi: Iran haitofumbia macho haki zake za nyuklia

Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa hapa mjini Tehran amesema leo kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitafumbia macho haki zake za nyuklia kwenye mazungumzo yanayoendelea kati yake na kundi la 5+1. Akiwahutubia Waislamu kwenye hotuba ya pili ya Sala ya Ijumaa hapa Tehran, Hujjatul Islam Kazem Siddiqi amesema timu ya mazungumzo ya Iran inajua vyema mstari mwekundu uko wapi kwenye mazungumzo hayo na kwamba Wamagharibi hawana haki ya kuitwisha Iran matakwa na mitazamo yao.
Sheikh Kazem Siddiqi amesema, makubaliano ya mwisho kati ya Iran na Wamagharibi sharti yatambue rasmi haki ya Iran ya kurutubisha urani ndani ya nchi pamoja na kustafidi na teknolojia ya nyuklia kwa malengo ya amani. Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa hapa Tehran pia amezungumzia masuala mengine ya kieneo na kimataifa kwenye hotuba yake hiyo lakini kubwa zaidi ni kuhusu suala la kujiimarisha kijeshi taifa la Iran kwa lengo la kujiweka tayari kujibu hujuma zozote za maadui. Kuhusiana na hilo Hujatul Islam Siddiqi amesema nia ya Iran ya kujiimarisha kijeshi si kuzitisha nchi majirani bali lengo lake kuu ni kuhakikisha taifa liko tayari wakati wote kukabiliana na hujuma zozote za maadui.

No comments: