Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 16, 2014

Kikwete: Vifo vya wanawake wajawazito TZ viko juu

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema kuwa, nchi yake imefanikiwa kupunguza vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano lakini akakiri kwamba idadi ya vifo vya akina mama wajawazito bado iko juu. Rais Kikwete amesema Tanzania inaweza kufikia malengo mengi ya milenia kufikia mwaka ujao wa 2015 iwapo sekta zote za serikali na zile za kibinafsi zitashirikiana. Kiongozi huyo amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika sekta ya afya lakini akasisitiza kuwa, bado kuna kibarua cha ziada kinachopaswa kufanywa ili kuimarisha zaidi utoaji huduma katika sekta hiyo.

Umoja wa Mataifa ulianzisha mpango wa Malengo ya Milenia mwaka 2000 ambapo nchi zote za dunia zilikubali kuweka mikakati ya kufikia malengo 8 ya milenia ifikapo mwaka 2015. Miongoni mwa malengo hayo ni kupunguzwa umasikini kwa asilimia 50 katika kila nchi, kupunguzwa kabisa maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi pamoja na kupanuliwa sekta za afya na elimu ili watu wengi zaidi waweze kwenda shule pamoja na kupata huduma bora za afya kote duniani.

No comments: