Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, May 14, 2012

Jimbo la New South Wales la Australia kutumia mfumo wa fedha wa Kiislamu

Wakuu wa jimbo la New South Wales la nchini Australia wana mpango wa kutumia mfumo wa kifedha wa Kiislamu katika jimbo lao.

Afisa mmoja wa serikali ya Australia amesema kuwa, ujumbe wa wataalamu wa huduma za taifa ukiongozwa na Barry O'Farrell, gavana wa mkoa wa New South Wales, wataelekea mjini Dubai Imarati Jumanne wiki hii kwa ajili ya kufanya mazungumzo na viongozi wa Shirika la Maendeleo ya Usafirishaji Nje Bidhaa la Dubai kuhusu masuala ya kisheria na usimamiaji, ya mfumo wa fedha wa Kiislamu.
Afisa huyo wa serikali ya Australia ambaye hakutaka jina lake litajwe ameliambia Shirika la Habari la Reuters kuwa, ujumbe huo utazungumza na maafisa wa shirika hilo la Imarati juu ya fursa mbalimbali za kibiashara zilizoko katika mkoa huo wa New South Wales na kuwataka wawekezaji wa Kiislamu kulipa umuhimu maalumu jimbo hilo.
Kwa upande wake, Bw. Salim Farrar, mwalimu wa sheria katika Chuo Kikuu cha Sydney, mji mkuu wa Australia amesema kuwa, inabidi serikali ya nchi hiyo iingilie kati ili kuhakikisha kunapasishwa sheria kuhusu uwekezaji wa Kiislamu nchini Australia.
Naye Bw. Talal Yasin, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Crescent Wealth, ambalo ni la kwanza la Kiislamu nchini Australia na ambalo lina makao yake mjini Sydney amesema kuwa mfumo wa kifedha wa Kiislamu unazidi kupata nguvu katika jamii ya wafanyabiashara nchini Australia.

No comments: