Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 16, 2014

Pengo kati ya matajiri na masikini lapanuka Uingereza

Ofisi ya Takwimu za Taifa nchini Uingereza (ONS) imetoa ripoti inayoonyesha kuwa, pengo kati ya tabaka la watu matajiri na lile la watu masikini linazidi kupanuka kwa kasi. ONS imesema hali hiyo inatia wasiwasi kwani mlingano katika jamii unazidi kupotea. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, matajiri wanazidi kuwa matajiri na masikini wanazidi kuzama kwenye lindi la uchochole.
Wataalamu wa masuala ya uchumi wanasema hali kama hiyo inaweza kusababisha ukosefu wa hali ya usalama na chuki za kitabaka. Pia uchumi unaweza kuathiriwa na hali kama hiyo haswa inapojitokeza kwamba masikini ni wengi kuliko matajiri.
Nchi nyingi za Magharibi ambazo zimeshindwa kudhibiti mlingano wa kitabaka kati ya matajiri na masikini zinakabiliwa na matatizo mengi hususan suala la usalama kama vile kuongezeka vitendo vya ujambazi na mauaji ya kiholela. Marekani ni miongoni mwa nchi zinazosumbuliwa mno na tatizo hilo.

No comments: