Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 16, 2014

'Uchaguzi Malawi utakuwa huru'

Tume ya uchaguzi ya Malawi imewahakikishia raia wa nchi hiyo pamoja na jamii ya kimataifa kwamba uchaguzi mkuu wa Mei 20 utakuwa huru na wa haki. Mwenyekiti wa tume hiyo, Maxon Mbendera amekanusha baadhi ya madai ya wapinzani kwamba tume hiyo huenda ikashirikiana na chama tawala kufanya uchakachuaji huku akisisitiza kuwa, teknolojia za kisasa zitatumika kwenye zoezi la upigaji kura ili kuondoa uwezekano wa kufanyika udanganyifu.
Raia milioni 7.5 wamejiandikisha kupiga kura katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika. Uchaguzi mkuu wa Mei 20 utatoa fursa kwa wananchi wa Malawi kumchagua rais, wabunge na madiwani. Kiti cha urais kimewavutia wagombea 12 akiwemo Rais Joyce Banda. Uchunguzi wa maoni unaonyesha kuwa, umaarufu wa Rais Banda umepungua mno na huenda akashikilia nafasi ya tatu. Kiongozi huyo amepuuzilia mbali uchunguzi huo wa maoni akisema umefadhiliwa na wapinzani ili kuwatamausha wafuasi wake.

No comments: