Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 17, 2014

Obama atishia kuzidisha vikwazo dhidi ya Russia

Kwa Mara nyingine tena Rais Barack Obama wa Marekani amedai kuwa ataweka vikwazo vikali zaidi kwa Russia. Obama ametoa madai hayo kupitia mazungumzo ya simu na Rais Francois Hollande wa Ufaransa kuhusiana na kadhia ya Ukraine, ambapo sambamba na kuisifu serikali ya Kiev, Ukraine kwa kuchukua hatua za lazima kwa ajili ya kuitisha uchaguzi wa rais wa nchi hiyo inayokabiliwa na tishio la kugawika, amekariri tena vitisho vyake dhidi ya Russia.
Aidha katika mazungumzo hayo ya simu kati ya marais hao wa Marekani na Ufaransa wamejadili kuhusu kikao kilichopangwa kufanyika mjini Paris kwa lengo la kujadili njia za kukabiliana na kundi la Boko Haram la nchini Nigeria. Vitisho vya Obama dhidi ya Russia, vimetolewa ikiwa ni siku moja tu ambapo John Kerry, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ameitaka Russia kuiruhusu Ukraine kuendesha uchaguzi wa rais katika tarehe iliyopangwa. Hata hivyo vitisho hivyo vinaonekana havina taathira yoyote kwa serikali ya Rais Vladimir Putin wa Russia na vinaonekana ni kama kelele za chura zisizoweza kumzuia ng'ombe kunywa maji.

No comments: