Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 9, 2013

‘Waasi na jeshi la Mali wametenda jinai dhidi ya raia’

Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limesema kuwa, waasi wa Tuareg pamoja na jeshi la Mali wametenda jinai na ubaguzi dhidi ya raia wa makundi tofauti ya nchi hiyo. Katika ripoti yake shirika hilo limesema kuwa, wanajeshi wanawatesa Watuareg huku waasi nao wakiripotiwa kuwazingira na kuwapiga mahasimu wao ambao wana ngozi nyeusi. Taarifa hiyo pia imeeleza kuwa, haki za binadamu za raia wa Mali zinakiukwa na askari jeshi wa nchi hiyo na pia makundi ya waasi. Kwa sababu hiyo Human Rights Watch imezitaka pande zinazopigana nchini Mali kuheshimu sheria za vita na kujiepusha na kuwashambulia raia. Huko nyuma pia Shirika la Msamaha Duniani Amnesty International lilisema kuwa, makundi yenye silaha hasa jeshi la Mali ambalo lilikuwa likisaidiwa na vikosi vya Ufaransa yanakiuka haki za binadamu, huku baadhi ya vitendo vikiweza hata kuitwa  jinai za vita.

Mgogoro nchini Mali ulianza Machi mwaka jana baada ya mapinduzi ya kijeshi, lakini ulishadidi na kupanuka baada ya Ufaransa kushambulia kaskazini mwa nchi hiyo kwa kisingizio cha kupambana na waasi.  

No comments: