Rais Macky Sall wa Senegal ameonya kuhusu mgogoro katika nchi za
eneo la Sahel barani Afrika bado haujamalizika. Sall amesema hayo
katika mahojiano na gazeti la Kifaransa la Le Figaro linalochapishwa
mjini Paris, na kuhusu hali ya kisiasa na kiusalama ya Mali ameeleza ana
matumaini kuwa uchaguzi utafanyika mwishoni mwa mwezi wa Julai, kwa
ushirikiano wa jamii ya kimataifa na Jumuiya ya Kiuchumi ya Magharibi
mwa Afrika ECOWAS. Matamshi ya Macky Sall yametolewa huku mazungumzo
kati ya wawakilishi wa serikali ya mpito ya Mali na kundi la kikabila la
Tuareg juu ya upigaji kura katika mji wa Kidal yakianza leo Juni 8
katika mji mkuu wa Burkina Faso,Ouagadougou.
Hii ni katika hali ambayo, mapigano ya jeshi la nchi hiyo na Harakati ya Kitaifa ya Ukombozi wa Azawadi kaskazini mwa nchi, ni awamu mpya ya mgogoro huo ulioenea hadi katika nchi nyingine za eneo la Sahel. Eneo la Sahel la Afrika linazijumuisha nchi za Algeria, Chad, Senegal, Mauritania, Niger na Mali, ambazo zina makundi tofauti ya kabila la Tuareg yanayoishi kwa kuhama hama kwenye maeneo hayo. Maisha ya kuhamahama na ya kiasili ya Watuareg yamelifanya kabila hilo kuingia na kutoka kwa urahisi katika mipaka ya nchi za eneo hilo. Baadhi ya makundi ya kabila hilo yanajishughulisha na magendo ya madawa ya kulevya na binadamu pamoja na kuwatekaji nyara raia wa kigeni.
Hii ni katika hali ambayo, mapigano ya jeshi la nchi hiyo na Harakati ya Kitaifa ya Ukombozi wa Azawadi kaskazini mwa nchi, ni awamu mpya ya mgogoro huo ulioenea hadi katika nchi nyingine za eneo la Sahel. Eneo la Sahel la Afrika linazijumuisha nchi za Algeria, Chad, Senegal, Mauritania, Niger na Mali, ambazo zina makundi tofauti ya kabila la Tuareg yanayoishi kwa kuhama hama kwenye maeneo hayo. Maisha ya kuhamahama na ya kiasili ya Watuareg yamelifanya kabila hilo kuingia na kutoka kwa urahisi katika mipaka ya nchi za eneo hilo. Baadhi ya makundi ya kabila hilo yanajishughulisha na magendo ya madawa ya kulevya na binadamu pamoja na kuwatekaji nyara raia wa kigeni.
Mgogoro wa Mali ulioanza mwezi Machi mwaka uliopita baada ya
mapinduzi ya kijeshi, yaliyoandaa mazingira ya kudhibitiwa eneo la
kaskazini mwa nchi hiyo na Harakati ya Kitaifa ya Ukombozi wa Azawad na
baadhi ya makundi yenye silaha yenye mfungamano na Watuareg. Kwa kutumia
kisingizio hicho Rais Francois Hollande wa Ufaransa Januari 11
aliivamia kaskazini mwa Mali kwa madai ya kupambana na ugaidi. Kushindwa
wanajeshi wa Ufaransa katika mapigano dhidi ya makundi ya upinzani
yenye silaha kaskazini mwa Mali kuliilazimu Paris itangaza muda wa
kuondoa askari wake magharibi mwa Afrika. Hata hivyo kubakia askari
1,000 wa Ufaransa kaskazini mwa Mali kwa kizingizio cha kushirikiana na
askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa, kunadhihirisha jitihada za
Paris za kuendelea kuweko kijeshi magharibi mwa Afrika. Vilevile
kuruhusu askari wa Ufaransa harakati ya Azawadi kwa mara nyingine
idhibiti mji muhimu wa Kidal ni aina fulani ya uingiliaji wa Paris
katika masuala ya ndani ya Mali. Ni wazi kuwa Ufaransa imeingilia
masuala ya Mali kwa ajili ya kudhamini maslahi yake haramu katika eneo
la Sahel. Vita nchini Mali ambayo vimepanuka hadi kwenye mipaka ya
Niger, vimesababisha kusimama shughuli za shirika la kifaransa la Areva
za kuzalishaji tani 350 za urani nchini Niger. Ufaransa inafanya
jitihada ya kuendelea kudhiniti eneo la kaskazini mwa Mali kwa kutumia
baadhi ya makundi kama vile harakati ya Azawadi , ili kulinda maslahi
yake haramu kwenye eneo la Magharibi mwa Afrika.
No comments:
Post a Comment