Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 9, 2013

Mandela alazwa tena hospitali baada ya kuzidiwa

Mzee Nelson Mandela rais wa kwanza wa Afrika Kusini baada ya utawala wa ubaguzi wa rangi amelazwa tena hospitali akisumbuliwa na maradhi ya mapafu. Taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais imeeleza kuwa, hali yake ni mbaya lakini imedhibitiwa na kwamba anaweza kupumua mwenyewe, suala linaloleta matumaini.  Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Mandela mwenye umri wa miaka 94 ambaye mwezi Aprili alilazwa hospitalini kutokana na matatizo ya kupumua, amekuwa akisumbuliwa tena na ugonjwa huo katika siku kadhaa zilizopita. Taarifa hiyo imeongeza kuwa, leo asubuhi Mzee Mandela alipelekwa hospitali mjini Pretoria baada ya kuzidiwa na kwamba madaktari wanafanya jitihada za kumtibu ili apate nafuu.
Rais Jacob Zuma kupitia mtandao wa tweeter amesema kwa niaba ya wananchi wa Afrika Kusini kwamba anamuombea mzee Madiba apate afueni haraka na kuvitaka vyombo vya habari na umma kwa ujumla kuheshimu faragha ya rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini na familia yake.

No comments: