
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Misri ametangaza kwamba usalama umeimarishwa nchini humo ambapo kumeongezwa idadi ya askari kwa ajili ya kulinda usalama katika vituo vya kupigia kura pamoja na ofisi za kampeni za uchaguzi na hali hiyo itaendelea hadi matokeo yatakapotangazwa. Uchaguzi huo utafanyika leo na kesho katika maeneo yote ya Misri.
Mwishoni mwa kampeni zake za uchaguzi Morsi amesema kwamba iwapo kura zitaibiwa basi kutatokea mapinduzi mengine makubwa nchini Misri dhidi ya watenda jinai ambayo yataendelea hadi pale malengo ya mapinduzi ya Januari 25 yatakapofikiwa.
No comments:
Post a Comment