Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 22, 2013

Msikiti wa Washia walengwa na mashambulizi Pakistan

Watu wasiopungua 15 wameuawa na wengine zaidi ya 24 kujeruhiwa vibaya katika shambulio la bomu lililofanywa katika msikiti wa Washia na katika seminari ya kidini katika mji wa Peshawar huko kaskazini magharibi mwa Pakistan. Maafisa wa usalama wa Peshawar wameeleza kuwa shambulizo hilo lilitekelezwa wakati waumini wa Kishia walipokuwa katika sala ya Ijumaa. Duru za kitiba pia zimearifu kuwa idadi ya waliouawa katika shambulio hilo inatazamiwa kuongezeka kwa kuzingatia kuwa hali ya baadhi ya majeruhiwa ni mbaya sana. 

Hadi hivi sasa hakuna kundi lolote lililotangaza kuhusika na mlipuko huo wa bomu. Mlipuko wa leo katika msikiti wa Washia huko Peshawar ni mkubwa zaidi kuwahi kutokea katika mji huo tangu serikali mpya ya Pakistan iingie madarakani mwezi Mei mwaka huu.  

No comments: