Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

Wafungwa wa Kimisri wafanya mgomo wa kula

Maelfu ya wafungwa wa Kimisri wameanza kufanya mgomo wa kula wakilalamikia hali mbaya iliyoko kwenye magereza ya nchi hiyo. Haytham Abu Khalil Msemaji wa 'harakati ya wafungwa wa kisiasa katika jela za Misri' amesema kuwa, zaidi ya wafungwa elfu ishirini na tano wanaoshikiliwa kwenye jela 114 na korokoroni kwenye maeneo mbalimbali nchini humo, wameanza kufanya mgomo wa kula wakilalamikia hali mbaya kwenye jela na magereza ya nchi hiyo. Abu Khalil amesema kuwa, mgomo huo utaendelea kwa wiki nzima kwa shabaha ya kuifahamisha jamii ya kimataifa matatizo yanayowakabili wafungwa hao.
Wakati huohuo, maelfu ya wananchi wa Misri ambao si wafungwa nao, wameanza kufanya mgomo wa kula ikiwa ni hatua ya kuwaunga mkono watoto na ndugu zao walioko jela. Wakati huohuo, Rais Adly Mansour wa serikali ya mpito ya Misri amebatilisha amri iliyotolewa hapo awali na Mohammad Morsi rais aliyeondolewa madarakani ya kuwasamehe viongozi na wanachama wa ngazi za juu wa Ikhwaanul Muslimiin na wanaharakati wengine wa Kiislamu nchini humo.

No comments: