Sergei Lavrov Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Russia kwa mara nyingine
tena ametaka Dakta Hassan Rohani Rais mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran ashiriki kwenye mkutano wa kimataifa wa Geneva 2 utakaojadili
kadhia ya Syria. Lavrov amesisitiza kuwa, Moscow inaamini kwamba kuna
ulazima mkubwa wa Dakta Rohani kushiriki kwenye mkutano huo. Waziri wa
Mambo ya Nchi za Nje wa Russia ameongeza kuwa, Iran na hali kadhalika
nchi zote zinazopakana na Syria ambazo zinafungamana na mgogoro wa nchi
hiyo na hata zile zinazowapatia hifadhi wakimbizi wa Syria, zinapaswa
kualikwa kwenye mkutano huo wa kimataifa utakaofanyika Geneva.
Lavrov
amebainisha kuwa, Ufaransa ambayo hadi wiki chache zilizopita ilikuwa
ikipinga vikali ushiriki wa Iran kwenye mkutano huo, hivi sasa imeamua
kubadilisha msimamo wake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment