Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, May 22, 2014

Haftar ataka serikali ya wakati wa mgogoro iundwe Libya

Jenerali mstaafu wa Libya, Khalifa Haftar aliyeanzisha vita dhidi ya makundi yenye silaha na kupinga serikali, ametaka mahakama iteue serikali ya wakati wa mgogoro itakayosimamia uchaguzi mpya nchini humo. Haftar pia ameituhumu serikali ya mpito ya Libya kuwa inaunga mkono ugaidi na kusema kuwa mapigano dhidi ya wanamgambo wenye silaha yataendelea.
Hayo yanajiri huku spika wa Bunge la Libya akiamuru kukamatwa wanajeshi walioasi na kushiriki katika mauaji ya umati ya raia katika mji wa Benghazi.
Nuri Abusahmin ambaye pia ni kamanda wa vikosi vyote vya ulinzi vya Libya amesema, serikali inafanya jitihada za kuzuia mapigano zaidi kati ya makundi yenye silaha nchini humo.
Siku ya Ijumaa Jenerali mstaafu Khalifa Haftar alitumia vikosi vya jeshi na helikopta kushambulia makundi ya wanamgambo katika mji wa Benghazi bila ruhusa ya serikali. Hii ni katika hali ambayo hadi sasa wanajeshi kadhaa wa Libya wameasi jeshi na kuungana naye.

No comments: