Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 14, 2014

Ujumbe wa Afrika Kusini wafanya safari mjini Tehran

Ujumbe wa kiuchumi na kibiashara, chini ya uongozi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini Bi Maite Nkoana-Mashabane uliondoka jana mjini Johannesburg, Afrika Kusini, kuja hapa mjini Tehran. Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Afrika Kusini, Mohammad Mojtaba Faraji, amesema kuwa, ujumbe huo unawashirikisha wanaharakati wa sekta tofauti kama vile madini, viwanda, uwekezaji, vyakula, kilimo, uchumi, biashara na mambo mengineyo.
Aidha Mojtaba, ameongeza kuwa, kwa kutumia fursa mbalimbali za uwekezaji na biashara kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Afrika Kusini, ujumbe huo unaweza kuinua kiwango cha uhusiano wa nchi mbili hizi. Mohammad Mojtaba Faraji, ameuzungumzia uhusiano wa nchi mbili katika sekta ya uichumi kuwa chanya na kwamba, Pretoria inaweza kutumia fursa iliyojitokea kwa ajili ya kuagiza bidhaa za Iran na wakati huo huo, Iran nayo kwa upande wake inaweza kuagiza bidhaa za nchi hiyo. Katika siku za hivi karibuni, nchi kadhaa za dunia zikiwemo zile za Ulaya zimekuwa zikifanya safari za mara kwa mara mjini Tehran na kusaini mikataba mbalimbali ya  kibiashara na kiuchuni.

No comments: