Mazungumzo ya siku ya kwanza kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA na ambayo hayakuhudhuriwa na vyombo vya habari yalifanyika jana alasiri huko mjini Vienna Austria.
Natija ya mazungumzo hayo yaliyodumu kwa muda wa saa tano na yaliyofanyika katika ofisi ya mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na karibu na ofisi ya Umoja wa Mataifa na ofisi nyingine za Kimataifa huko mjini Vienna, bado haijafahamika hadi sasa.
Mazungumzo hayo yameendelea hii leo kwa kuhudhuriwa na Ali Asghar Sultaniye Mjumbe wa kudumu wa Iran katika wakala huo na Herman Nackaerts Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IAEA.
Katika hali hiyo viongozi wa ngazi za juu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na wa IAEA wamefafanua kuwa, wameamua kukaa katika meza ya mazungumzo kutokana na kuwepo mitizamo chanya ya kufikiwa maelewano kati ya pande mbili hizo.
Kuna nukta mbili muhimu ambazo zinaweza kuyafanya mazungumzo kati ya Iran na IAEA kuwa yenye natija nzuri na ya kimantiki. Nukta ya kwanza ni uwazi wa wakala huo kwa Tehran katika fremu ya ushirikiano wa Mkataba wa Kuzuia Uzalishaji na Uenezwaji wa Silaha za Nyuklia NPT. Aidha ni vyema kukumbusha hapa kwamba, kwa mara kadhaa Iran imetoa nafasi kwa wakurugenzi wa IAEA kutembelea kituo chake cha kijeshi cha Parchin kilichoko mashariki mwa Tehran, suala linaloonesha kwamba, shughuli za nyuklia za Iran zinafanyika kwa uwazi, malengo ya amani na kwa ushirikiano na wakala huo.
Ama nukta ya pili ni kuthibitishiwa Iran nia njema na uaminifu wa upande wa pili kuhusiana na shughuli zake za nyuklia. Hii ni kwa sababu kupuuzwa jambo hilo na nchi za Magharibi huko nyuma kumepelekea kutolewa ripoti zisizo na msingi na IAEA kuhusu miradi ya nyuklia ya Iran. Ni wazi kuwa iwapo nukta mbili hizo zitazingatiwa na pande husika, tunaweza kuwa na matumaini kuwa mazungumzo yajayo yatakuwa na natija nzuri kwa pande zote mbili.
Ama nukta ya pili ni kuthibitishiwa Iran nia njema na uaminifu wa upande wa pili kuhusiana na shughuli zake za nyuklia. Hii ni kwa sababu kupuuzwa jambo hilo na nchi za Magharibi huko nyuma kumepelekea kutolewa ripoti zisizo na msingi na IAEA kuhusu miradi ya nyuklia ya Iran. Ni wazi kuwa iwapo nukta mbili hizo zitazingatiwa na pande husika, tunaweza kuwa na matumaini kuwa mazungumzo yajayo yatakuwa na natija nzuri kwa pande zote mbili.
No comments:
Post a Comment