Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, July 18, 2015

Liverpool yamwinda Benteke

Klabu ya Liverpool nchini Uingereza imetoa kitita cha pauni milioni 32.5 kwa Aston Villa kwa lengo la kumsajili mshambuliaji wa Ubelgiji Christian Benteke.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alifunga mabao 12 katika mechi 12 katika msimu wa mwaka 2014-2015 na kuisadia Villa kusalia katika ligi kuu ya Uingereza.
Liverpool inamtaka mchezaji huyo baada ya kupokea kitita cha pauni milioni 49 kutokana na mauzo ya mchezaji Raheem Sterling aliyehamia Mancity.

Benteke bado amesalia na kandarasi ya miaka 2 katika klabu ya Villa.
Mshambuliaji wa Uingereza Daniel Sturridge aliichezea timu hiyo mara 18 msimu uliopita kutokana na msururu wa majeraha na atasalia nje hadi mwezi Septemba akiuguza jeraha la kiuno.


No comments: