Nigeria na nchi jirani zimeahidi kuunda kikosi cha askari 8,700
kukabiliana na kundi la kigaidi la Boko Haram ambalo limeeneza ugaidi
nje ya mipaka ya nchi hiyo. Katika taarifa iliyotolewa Jumamosi baada ya
kikao cha siku tatu huko Yaounde mji mkuu wa Cameroon, wawakilishi wa
Benin, Cameroon, Niger, Nigeria na Chad wameafiki kuunda kikosi cha
askari 8,700 kwa lengo la kukabiliana na Boko Haram.
Kufuatia uamuzi
huo, Umoja wa Afrika unatazamiwa kuwasilisha mpango wa kikosi hicho kwa
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuidhinishwa rasmi.
Kundi hilo la kitakfiri limeua watu zaidi ya 13,000 na kupelekea wengine
takribani milioni moja na nusu kuachwa bila makao tokea mwaka 2008.
Tayari wanajeshi wa Chad na Niger wameshatuma wanajeshi wao Nigeria kukabiliana na magaidi wa Boko Haram.
Duru za usalama zinadokeza kuwa kundi la Boko Haram lina magaidi sugu
karibu elfu sita. Huku hayo yakijiri Tume ya Uchaguzi Nigeria
imetangaza kuakhirisha uchaguzi wa rais na bunge uliokuwa umepangwa
kufanyika Februari 14. Uchaguzi huo umeakhirishwa hadi Machi 28 kwa
ajili wanajeshi wanaopambana na Boko Haram hawawezi kudhamini usalama wa
wapigaji kura kwa sasa.
No comments:
Post a Comment