Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

Wakuu wa ECOWAS wakutana kwa dharura Ghana

Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Magharibi mwa Afrika ECOWAS wameanza kikao cha dharura nchini Ghana, kwa shabaha ya kujadili migogoro na machafuko yanayozidi kupamba moto katika nchi za Mali na Nigeria. Taarifa hizo zinaeleza kuwa, kikao hicho kilianza jana mjini Accra na zinasema kuwa, wakuu wa ECOWAS wataendelea kujadili masuala muhimu kama vile migogoro ya kiusalama nchini Nigeria na Mali. Viongozi hao wameitaka jumuiya ya kimataifa iingilie kati suala la kutekwa nyara wanafunzi wasichana wanaozidi 270 wanaoshikiwa na kundi la Boko Haram la nchini Nigeria.
Rais Alassane Ouattara wa Ivory Coast amesema kuwa, wakuu wa ECOWAS wameujadili mgogoro wa Mali na hasa baada ya kushuhudiwa kuanza machafuko mapya kaskazini mwa nchi hiyo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, mwezi Machi uliopita, Rais Ouattara alikabidhi uenyekiti wa mzunguko wa jumuiya hiyo kwa Rais John Dramani Mahama wa Ghana.

No comments: