Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 3, 2014

Rwanda: HRW inawafanyia propaganda magaidi

Wizara ya Sheria ya Rwanda imelituhumu Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch kuwa ni msemaji wa makundi ya kigaidi na kufanya propaganda dhidi ya serikali ya Kigali. Taarifa iliyotolewa jana na Wizara ya Sheria ya Rwanda imelituhumu shirika hilo kuwa linabadilisha shughuli zake na kuwa msemaji wa makundi ya kigaidi na yenye kutenda jinai na hasa kundi la waasi wa Democratic Liberation Forces of Rwanda 'FDLR' la waasi wa Kihutu wa Rwanda walioko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. 
Serikali ya Rwanda inalituhumu kundi hilo kuwa limetenda jinai za mauaji ya kimbari yaliyotokea mwaka 1994 nchini humo. Wizara ya Sheria ya Rwanda imelikosoa vikali shirika la Human Rights Watch kwa kufanya propaganda chafu dhidi ya jeshi la polisi la Rwanda na kuulenga pia uhuru wa mfumo wa sheria wa nchi hiyo. Serikali ya Kigali imetishia kutoongeza muda wa protokali ya mashirikiano na shirika hilo. Inafaa kuashiria hapa kuwa, Rwanda na shirika la HRW zilitiliana saini makubaliano ya kushirikiana pande mbili katika masuala ya haki za binadamu mwaka 2011.

No comments: