Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, February 10, 2015

Rafsanjani: Wairani wanashikamana na Mapinduzi yao

Mkuu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Kiislamu wa Iran amesema kuwa, wananchi wa Iran watauthibitishia ulimwengu kwamba hawajayatupa mkono Mapinduzi ya Kiislamu kwa kujitokeza kwa wingi kwenye maandamano ya kesho ya kuadhimisha ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.

Akizungumza na wajumbe wa taasisi mbalimbali za wanachuo wa Chuo Kikuu cha Shahid Beheshti mjini Tehran, Ayatullah Hashemi Rafsanjani amesema kuwa, wananchi ndiyo rasilimali kuu ya kuendelea kuwepo Mapinduzi ya Kiislamu hapa nchini na kusisitiza kwamba kujitokeza umati mkubwa wa wananchi hapo kesho kutazima njama za maadui wa Mapinduzi ya Kiislamu. Wakati huohuo, Msaidizi wa Mkuu wa Baraza la Uratibu la Taasisi ya Ulinganiaji wa Kiislamu hapa nchini amesema kuwa, nara na kauli mbiu ya maandamano ya mwaka huu nchini kote ni 'Mauti kwa Marekani' na 'Labbayka ya Rasulallah'. Asghar Abkhazwar ameongeza kuwa, zaidi ya wageni 400 kutoka nchi 30 duniani watashiriki kwenye sherehe hizo. Ameongeza kuwa, kwa uchache  watu wasiopungua milioni nne wa mjini  Tehran na wengine zaidi ya milioni 45 nchini kote watashiriki kwenye maandamano ya hapo kesho.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, wananchi wa Iran wakiongozwa na Imam Ruhullah Khomeini MA waliuangusha utawala wa kifalme hapa nchini yapata miaka 36 na kuanzisha mfumo wa utawala wa Kiislamu.

No comments: