Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

Iran na Kuwait kujadili masuala ya Mashariki ya Kati

Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa Iran na Kuwait zitajadili matukio ya hivi karibuni katika Mashariki ya Kati wakati wa safari ya hapo kesho ya Mfalme wa Kuwait Sheikh Sabah al-Ahmad al-Jaber al-Sabah hapa nchini. Mohammad Ali Beik, Mkuu wa Idara ya Ghuba ya Uajemi katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema miongoni mwa ajenda zitakazojadiliwa na viongozi wa nchi mbili ni pamoja na ustawishaji wa ushirikiano wa pande mbili, ufatiliaji wa makubaliano yaliyofikiwa katika miaka michache iliyopita na mashauriano juu ya matukio ya eneo hususan Mashariki ya Kati.
Mohammad Ali Beik ameongeza kuwa wakati wa safari yake ya siku mbili hapa nchini, Mfalme wa Kuwait atakutana na kufanya mazungumzo na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei na Rais Hassan Rouhani. Aidha amesema Iran na Kuwait zitasaini pia hati tano za makubaliano na maelewano pamoja na kubadilishana hati za masuala ya usalama

No comments: