Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, July 14, 2013

Taliban ya Pakistan yaasisi kambi nchini Syria

Kundi la Taliban la nchini Pakistan limeasisi kambi nchini Syria ili kushirikiana na makundi ya kigaidi yanayofadhiliwa na nchi za kigeni katika mapigano dhidi ya serikali ya Rais Bashar al Assad wa nchi hiyo. Kamanda wa ngazi ya juu wa Taliban amesema kuwa kambi hiyo imeasisiwa na Tahriki Taliban Pakistan (TTP) kwa msaada wa wapiganaji wa zamani wa Kiafghani wenye asili ya Mashariki ya Kati waliohamia nchini Syria katika miaka ya hivi karibuni.
Mohammad Amin afisa wa Taliban na mratibu wa kambi hiyo waliyoiasisi huko Syria amesema kuwa wataalamu 12 wa masuala ya teknoloja ya habari wameelekea Syria miezi miwili iliyopita ili kutathmini hali ya mambo nchini humo. Amesema kazi ya kambi hiyo  iliyoasisiwa Syria miezi sita iliyopita,  ni kutathmini mahitaji ya makundi ya kigaidi yaliyoko huko na kuratibu oparesheni za pamoja dhidi ya serikali ya Damascus.

No comments: