Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 24, 2014

Yukiya Amano: Iran inaheshimu ahadi zake za nyuklia

Yukiya Amano, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA, amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaheshimu ahadi zake katika mwenendo mzima wa nyuklia. Amano ameyasema hayo mjini Vienna, Austria wakati akitoa ripoti ya wakala huo kuhusiana na kutekelezwa makubaliano kuhusu maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na miradi ya nyuklia ya Iran. Katika ripoti hiyo, imeelezwa kuwa Tehran hadi sasa imekwishachukua hatua kadhaa za kutekeleza kivitedo makubaliano yaliyofikiwa kati yake na wakala huo mwezi Februari mwaka huu.
Aidha katika ripoti hiyo Amano amesisitiza kuwa, tangu tarehe 20 mwezi huu, Iran haijarutubisha madini ya urani katika vituo vyake vyote, kwa zaidi ya asilimia tano inayotakiwa. Kwa mujibu wa ripoti hiyo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imechukua pia hatua za kivitendo kwa mujibu wa ushirikiano wa makubaliano yaliyofikiwa mwezi Novemba mwaka jana. Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA, amesema kuwa, Tehran na wakala huo zimefikia makubaliano matano mengine tarehe 20 mwezi huu na imepangwa kutekelezwa makuabaliano hayo kabla ya tarehe 25 mwezi Agosti mwaka huu.

No comments: