Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 24, 2014

Renamo: Msumbiji iweke mazingira mazuri ya uchaguzi

Kiongozi wa chama cha upinzani RENAMO nchini Msumbiji, Bwana Afonso Dhlakama, ameitaka serikali ya nchi hiyo kuandaa mazingira mazuri ya kufanyika uchaguzi mkuu. Dhlakama ameyasema hayo jana huku akiikosoa serikali ya Maputo kwa kukwamisha mwenendo wa uchaguzi na kuanza kampeni za uchaguzi huo mkuu uliopangwa kufanyika tarehe 15 Oktoba mwaka huu. Afonso amesema kuwa, ili aweze kushiriki katika uchaguzi huo, serikali ya Rais Armando Guebuza wa nchi hiyo, inatakiwa kwanza imdhaminie usalama wa kutosha wa kuendesha kampeni zake katika maeneo tofauti ya nchi.
RENAMO ni chama kikubwa chenye wawakilishi wengi bungeni nchini Msumbiji, huku ukiwa na viti 51 kati ya viti vyote 250 bungeni. Chama hicho kilitia saini makubaliano ya usitishaji vita mwaka 1992. Hata hivyo ilianzisha mashambulizi yake dhidi ya serikali hapo mwaka jana kwa madai kwamba serikali ya Rais Guebuza haikutekeleza uadilifu katika ugawaji wa mali za taifa hilo. Mwezi uliopita chama hicho kilisaini makubaliano ya awali na serikali ya Maputo ambapo kwa mujibu wa makubaliano hayo, waasi hao wa RENAMO watajiunga katika jeshi na polisi ya nchi hiyo. Hata hivyo ilisisitiza kuwa, hawataweka chini silaha hadi pale kutakapotiwa saini makubaliano ya mwisho na serikali.

No comments: