Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 24, 2014

Waandamana kumuunga mkono jenerali mstaafu Libya

Maelfu ya wananchi wamefanya maandamano nchini Libya wakimuunga mkono jenerali mstaafu wa nchi hiyo, Khalifa Haftar kutokana na juhudi zake za kurejesha amani nchini humo. Maandamano hayo yamefanyika katika medani kuu ya mjini Tripoli ambapo waandamanaji wameunga mkono hatua za jenerali huyo mstaafu za kupambana na makundi ya kigaidi ambayo yamekuwa yakifanya mashambulizi na jinai za kila mara nchini Libya, huku wakimtaka kukata kabisa mizizi ya ugaidi ndani ya ardhi ya nchi hiyo. Waandamanaji walibeba mabango yaliyokuwa na maandishi ya kumuunga mkono Khalifa Haftar.
Kwa upande mwingine waandamanaji hao wameituhumu Kongresi ya Taifa yaani bunge licha ya taasisi hiyo muhimu ya serikali kutangaza tarehe ya kufanyika uchaguzi wa bunge nchini Libya. Wapiganaji wa jenerali huyo mstaafu walianzisha mashambulizi dhidi ya makundi ya kigaidi mjini Benghazi mashariki mwa nchi hiyo kuanzia wiki iliyopita. Licha ya yeye kustaafu jeshini lakini hadi sasa bado anajihesabu kuwa ni mkuu wa jeshi la taifa la nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika. Wiki iliyopita alitangaza pia kuwa, ataisafisha Libya na vitendo vya ukatili, utumiaji mabavu na ugaidi.

No comments: