Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 23, 2014

Walimu Nigeria waandamana kupinga Boko Haram

Walimu nchini Nigeria wamefanya maandamano kupinga hatua ya kundi la Boko Haram, ya kuwateka nyara wanafunzi wa kike zaidi ya 200 huko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Maandamano hayo yalifanyika hapo jana mjini Maiduguri, makao makuu ya jimbo la Borno, ambapo pamoja na mambo mengine wamelaani mauaji dhidi ya walimu katika mashambulizi ya kundi hilo. Mkuu wa umoja wa walimu nchini Nigeria Bwana Michel Alogba Olukoya amesema kuwa, Boko Haram katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, limeua karibu walimu 173 nchini humo.
Katika maandamano hayo walimu walibeba mabango yaliyokuwa na maandishi yasemayo: "Turejesheeni mabinti zetu." Kwa mujibu wa ripoti ya polisi ya nchi hiyo, wanafunzi 276 wa shule ya sekondari ya jimbo la Borno walitekwa nyara hapo tarehe 14 Aprili mwaka huu na kundi la Boko Haram ambapo 53 kati yao walifanikiwa kutoroka. Kundi hilo lilitangaza kuhusika na tukio hilo. Hii ni katika hali ambayo serikali ya Abuja imekuwa ikikosolewa ndani na nje ya Nigeria kutokana na kushindwa kuwakomboa wasichana hao. Wakati huo huo, Umoja wa Mataifa umeliweka jina la kundi la Boko Haramu katika orodha ya makundi ya kigaidi duniani.

No comments: