Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 10, 2013

Magaidi 350 wajisalimisha kwa jeshi la Syria

Magaidi  350 wamejisalimisha kwa jeshi la Syria na kuweka chini silaha zao. Shirika la Habari la Syria (SANA) limetangaza kuwa magaidi hao wamejisalimisha kwa jeshi la nchi hiyo, katika mkoa wa Homs wa katikati mwa Syria. Magaidi hao waliokuwa wakifanya vitendo vya kigaidi dhidi ya wananchi na askari wa nchi hiyo mjini Homs, wamejisalimisha kwa pamoja kwa jeshi la taifa la Syria katika vijiji vya Tal Ashour, ar-Rabiia, Jadidul-as na at-Tambulah mkoani Homs.
Magaidi hao wameahidi pia kutobeba tena silaha au kufanya kitendo chochote kilicho dhidi ya usalama wa raia na wa taifa la Syria. Wakati huo huo, wapiganaji wanaojiita eti jeshi huru la Syria, wametangaza kuhusika katika mripuko wa bomu uliotokea katika mji mkuu wa Lebanon, Bairut. Bassam ad-Dada, mmoja wa viongozi wa eti jeshi huru la Syria amesema wapiganaji wa jeshi hilo ndio waliotega bomu hilo mjini Beirut, Lebanon. Mchana wa leo, gari lililokuwa limebeba mada za miripuko, limeripuka katika eneo la maegesho ya magari, karibu na ofisi za Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC na kuwajeruhi kwa uchache watu 30 na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali.

No comments: