Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 17, 2014

Waziri Mkuu mpya wa India asherekea ushindi

Melfu ya wafuasi wa chama cha Bharatiya Janata Party (BJP) nchini India wamejitokeza mabarabarani hii leo kusherehekea ushindi wa chama hicho katika uchaguzi mkuu. Narendra Modi, mgombea wa BJP aliyechaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa India ameungana na wafuasi wa chama hicho katika shehere hizo, waliokuwa wamejikusanya mjini Delhi kumlaki akitoka mkoani kwake Gujarat. Chama cha wahafidhina cha BJT kimekuwa cha kwanza nchini humo kushinda uchaguzi kwa wingi wa kura ikiwa ni baada ya miongo mitatu.
Chama hicho cha upinzani kilikishinda chama kilichokuwa madarakani cha Congress Party kwa kujinyakulia zaidi ya viti 273 vya bunge vinavyotakiwa ili kuunda serikali.
Tangu mwaka 1989 India imekuwa ikiongozwa na serikali ya muungano wa vyama kadhaa, lakini waziri mkuu mtarajiwa Narendra Modi hatolazimika kufanya hivyo, kwa kuwa chama chake kimeshinda viti vya kutosha bungeni vitakavyomuwezesha kuunda serikali inayojitegemea.
Akiwahutubia wafuasi wake mjini New Dehli Modi amesema, serikali yake itafanya jitihada za kuanzisha fursa mpya za kazi, kuleta maendeleo na kuwa na uwazi katika siasa zake.

No comments: