Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 17, 2014

Ban awataka Waguinea Bissau washiriki uchaguzi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito kwa wananchi wa Guinea Bissau wajitokeze kwa wingi kushiriki katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais wa nchi hiyo. Ban Ki-moon amewataka wananchi wa Guinea Bissau wathibitishe itikadi zao na kutekeleza jukumu lao kama raia kwa kushiriki duru hiyo ya pili ya uchaguzi wa rais itakayofanyika hapo kesho Jumapili.

Uchaguzi huo unatarajiwa kuhitimisha duru ya mpito nchini humo. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  pia amevishukuru vyama vyote vya siasa vya Guinea Bissau na pia wagombea wawili wa uchaguzi huo kwa kufanya kampeni za uchaguzi kwa amani.
 Wagombea wawili ambao ni Jose Mario Vaz Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo na Nuno Gomes Nabiam mgombea wa kujitegemea ndio watakaochuana katika duru hii ya pili ya uchaguzi huo baada ya kuongoza katika duru ya kwanza ya uchaguzi uliofanyika Aprili 13.

No comments: