Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 17, 2014

Mwafaka wa muundo wa serikali wafikiwa Palestina

Afisa mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina HAMAS amesema harakati hiyo na ile ya Fat’h zimefikia makubaliano kuhusu muundo wa serikali ya maridhiano ya kitaifa. Mussa Abu Marzouq, Naibu Mkuu wa Idara ya Kisiasa ya HAMAS amesema harakati hiyo imeridhishwa na maafikiano yaliyofikiwa na kuongeza kwamba baada ya kushauriana na Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, Azzam Al Ahmad, afisa mwandamizi wa Fat’h ataelekea Ukanda wa Gaza mwishoni mwa wiki hii kwa ajili ya kukamilisha mabadiliko ya mwisho yanayopasa kufanywa katika makubaliano hayo ya pande mbili.
Abu Marzouq ameashiria pia uingiliaji mkubwa uliofanywa na madola ya nje katika mchakato wa maridhiano ya kitaifa ya Wapalestina na kueleza kwamba matumaini yake ni kuona uingiliaji huo hauvurugi makubaliano yaliyofikiwa hadi sasa. Tarehe 23 ya mwezi uliopita wa Aprili, harakati za Palestina za Fat’h na HAMAS zilisaini makubaliano ya utekelezaji hati ya maridhiano iliyosainiwa na pande mbili huko mjini Cairo, Misri na taarifa ya Doha, Qatar, ambapo kwa mujibu wa hati hizo, harakati hizo ziliahidi kufanya juhudi za kumaliza mpasuko uliojitokeza baina ya makundi ya Kipalestina na kuendelea kwa takribani miaka saba sasa

No comments: