Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 24, 2014

Mahakama Kuu Malawi yatupilia mbali ombi la Banda

Mahakama Kuu nchini Malawi imetupilia mbali ombi la Rais Joyce Banda wa nchi hiyo la kutaka kuzuia kutangazwa matokeo ya uchaguzi nchini humo. Jaji Mkuu wa mahakama hiyo Mike Tembo amesema kuwa, malalamiko ya Rais Banda kabla ya kutangazwa matokeo rasmi, hayana msingi wowote. Hii ni katika hali ambayo chama cha Rais Banda juzi kilidai kuwa, idadi ya wapiga kura katika baadhi ya maeneo, ilikuwa haiendani na idadi ya majina ya watu waliojiandikisha na kwamba kulikuwa na utata pia katika makaratasi ya kupigia kura sambamba na kudukuliwa kompyuta za kuhesabu kura.
Kwa mujibu wa waangalizi wa uchaguzi huo, na ingawa yalikuwepo mapungufu ya kiidara lakini uchakachuaji ulikuwa mdogo. Wakati huo huo, Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini Malawi, Maxon Mbendera, amekataa ombi la Rais Joice Banda la kutaka kuhesabiwa upya kura na kuongeza kuwa, ombi hilo la Banda limekuja kutokana na kukata kwake tamaa ya kushindi katika uchaguzi huo uliofanyika siku ya Jumanne. Huo ni uchaguzi wa tano tangu Malawi ilipoanzisha mfumo wa vyama vingi mwaka 1994.

No comments: