Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, May 21, 2014

Ufaransa yaakhirisha kuondoa askari wake nchini Mali

Ufaransa imeakhirisha mpango wa kuondoa vikosi vyake nchini Mali, ikidai kuwa uamuzi huo umesababishwa na machafuko yaliyoshuhudiwa hivi karibuni nchini humo. Duru za ulinzi za Ufaransa zimesema kuwa, mpango wa huko nyuma wa kuwapeleka askari wa nchi hiyo walio nchini Mali katika nchi nyingine za Kiafrika umeakhirisha, baada ya kushuhudiwa machafuko hivi karibuni kati ya jeshi na wanamgambo katika mji wa kaskazini wa Kida.

Mwanzoni mwa mwezi huu Paris ilisema kuwa imepanga kuwaondoa nchini Mali askari 2000 kati ya 3000 walioko nchini humo na kuwapeleka katika nchi nyingine za eneo la Sahel.
Katika upande mwingine Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani mapigango ya hivi karibuni nchini Mali na kutaka machafuko hayo yakomeshwe mara moja.

No comments: