Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, May 21, 2014

Mashirika: Lebanon isiwarejeshe wakimbizi Palestina

Taasisi 8 za haki za binadamu zimewataka maafisa wa Lebanon kuacha kuwarejesha wakimbizi wa Palestina wanaokimbia mgogoro wa Syria. Taasisi hizo zikiwemo Kituo cha Haki za Binadamu cha Lebanon, Taasisi ya Haki za Binadamu ya Palestina na Mtandano wa Haki za Bindamu wa Ulaya na Mediterranean zimesema kuwa, katika hali ambayo ni rahisi kwa Wasyria wanaokimbia machafuko kuingia Lebanon, kumeripotiwa matukio kadhaa ya kuwazuia wakimbizi wa Palestina wanaokimbia vita Syria kuingia na kupata hifadhi nchini Lebanon.

Taasisi hizo zimeashiria kufukuzwa nchini Lebanon wakimbizi wa Palestina wanaotokea Syria mwezi huu wa Mei na kusema kuwa hatua hiyo ni kinyume na Mkataba wa Umoja wa Mataifa unaopinga mateso. Maafisa wa Lebanon wametakiwa na taasisi hizo za kutetea haki za binadamu kuwapa haki wanazostahili wakimbizi wa Palestina wanaotokea Syria sawa na wanavyofanya kwa wakimbizi wa Syria.

No comments: