Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Somalia yaiomba Ethiopia iisaidie kulinda wageni

Serikali ya Somalia imeitaka serikali ya Ethiopia iisaidie kuwalinda wanadiplomasia wa kigeni pamoja na wafanyakazi wa mashirika ya misaada ya kibinadamu. Buri Muhammad Hamza, Mshauri Mkuu wa Rais wa Somalia ametoa ombi hilo alipokutana na kufanya mazungumzo na Wondimu Asamnenu balozi wa Ethiopia mjini Mogadishu na kusisitiza kwamba, wanaitaka serikali ya Addis Ababa ishiriki katika kudhamini ulinzi na usalama wa wafanyakazi wa mashirika ya utoaji misaada ya kibinaadamu pamoja na wanadiplomasia wa kigeni walioko nchini humo.
Aidha Buri Hamza amesema katika mazungumzo yake na balozi huyo wa Ethiopia kwamba, hadi sasa Addis Ababa imekuwa mwenyeji wa mikutano kadhaa ya amani na usalama nchini Somalia na vile vile kuna maelfu ya Wasomalia waliokimbia nchini Ethiopia na kuomba hifadhi huko kutokana na nchi yao kukabiliwa na machafuko. Mshauri Mkuu wa Rais wa Somalia ambaye pia ni msemaji wa Rais ameongeza kuwa, wanajeshi wa Ethiopia wanashirikiana na vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Afrika AMISOM katika kupambana na wanamgambo wa al-Shabab hali inayoonesha kuweko ushirikiano mzuri kati ya Mogadishu na Addis Ababa.

No comments: