Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

B/Wawakilishi ZNZ lataka kero za Muungano zitatuliwe

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wameitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), kuzipatia ufumbuzi kero za Muungano, ambazo baadhi yake zimekuwa zikirudisha nyuma maendeleo ya wananchi na kukwamisha juhudi za kupambana na umasikini. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyeviti wa Wenyeviti wa Baraza la Wawakilishi, Hamza Hassan Juma, wakati akisoma taarifa ya kamati yake pamoja na kuchangia Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2014-2015 katika Baraza la Wawakilishi.
Hamza Hassan Juma amesema kuwa, wananchi wamekuwa wakisikitishwa na kuwepo kwa vikwazo vya biashara katika maeneo ya Tanzania Bara na Zanzibar na hivyo kurudisha nyuma shughuli zao za kibiashara, usafirishaji wa mizigo na uingizaji. Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamezitaka serikali zote mbili kuharakisha kuondosha usumbufu wa wafanyabiashara katika kuingiza bidhaa mbalimbali katika Bandari ya Dar es Salaam na Malindi iliyopo Unguja. Inaelezwa kuwa, wafanyabiashara wadogo, wakiwemo wanawake, wamevunjika moyo na wengine kuacha kufanya shughuli za kibiashara, kwa sababu ya vikwazo vya ushuru mkubwa kwa watendaji wa kodi za mapato.

No comments: