Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Mazungumzo ya amani S/Kusini kufanyika mwezi ujao

Mazungumzo ya amani ya Sudan Kusini yamesogezwa mbele na sasa yatafanyika mwezi ujao wa Juni.  Mtandao wa Habari wa al-Yaums Sabi'i umeinukuu ya Jumuiya ya kieneo ya Mashariki mwa Afrika IGAD Iikitangaza kwamba, pande mbili hasimu huko Sudan Kusini zitakutana tena katika mazungumzo ya amani tarehe 4 ya mwezi ujao wa Juni.
Taarifa ya IGAD imebainisha kwamba, imezitaka pande zinazozozan huko Sudan Kusini kuunda kamati mbili za kisiasa na kiusalama.
Aidha Jumuiya ya kieneo ya Mashariki mwa Afrika IGAD imesisitiza juu ya udharura wa kuheshimiwa makubaliano ya usitishaji vita nchini Sudan Kusini.
Kufuatia mashinikizo ya kimataifa vikosi vya serikali ya Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini na wanamgambo watiifu kwa kiongozi wa waasi Riek Machar hivi karibuni walilazimika kutia saini makubaliano ya amani mjini Addis Abbas Ethiopia, lakini bado vipengee vya makubaliano hayo havijatekelezwa ipasavyo.

No comments: