Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 24, 2014

Ugonjwa wa Ebola waua watu 101 Guinea Conakry

Wizara ya Afya nchini Guinea, imetangaza kuwa, watu 101 wamepoteza maisha yao kutokana na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola. Kwa mujibu wa wizara hiyo, takwimu hizo ni za kuanzia mwezi Januari mwaka huu hadi sasa. Aidha wizara hiyo imesema, watu wengine wanane wamekumbwa na ugonjwa huo hivi karibuni katika eneo la mpaka kati ya Guinea na Liberia katika mji wa Telimele wamagharibi mwa nchi hiyo. Asilimia 90 ya waathirika wa virusi vya ugonjwa wa Ebola, hufariki dunia suala lililopelekea ugonjwa huo kutajwa kuwa wa hatari zaidi.
Mwezi Machi mwaka huu, virusi vya Ebola viliripotiwa kushuhudiwa katika nchi za Liberia, Sierra Leone na Mali. Baadhi ya nchi jirani na mataifa hayo zilichukua hatua kali za kuzuia maambukizi ya virusi hivyo ikiwa ni pamoja na kufunga mipaka na hata kuzuia safari za ndege kutoka nchi hizo. Hata hivyo juhudi kubwa zilizochukuliwa na nchi hizo kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO), zinatajwa kuwa ndiyo sababu ya kupungua maambukizi na ongezeko la kuenea virusi vya ugonjwa huo.

No comments: