Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 17, 2014

Saudia,Qatar,Uturuki zazidi kushirikiana na magaidi

Duru za Lebanon zimearifu kwamba, nchi za Saudia, Qatar na Uturuki zimeendelea kushirikiana kijeshi na kitaarifa na magaidi wanaopigana dhidi ya serikali ya Rais Bashar al-Assad wa Syria. Ripoti hizo zinabainisha kwamba, idadi kadhaa ya maafisa wa kiusalama wa Saudi Arabia, Qatar na Uturuki wamekuwa wakishirikiana kikamilifu na magaidi huko Syria.
Gazeti la Lebanon la al-Jamhuriyah limefichua kwamba, hata kuna maafisa wa ngazi za juu wa kijeshi wa Saudia, Qatar na Uturuki ambao wako nchini Syria. Aidha gazeti hilo linabainisha zaidi kwamba, miongoni mwa magaidi waliouawa nchini Syria kuna maafisa wa kiusalama wa Saudia na Qatar na kwamba, hivi sasa Riyadh na Doha zinafanya juhudi za kurejeshwa viwiliwili hivyo ili vikazikwe katika nchi zao. Machafuko nchini Syria yalianza mwaka 2011 na serikali ya Damascus inazilaumu nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani, Uingereza na Ufaransa pamoja na waitifaki katika eneo yaani Saudi Arabia, Uturuki, Qatar na utawala wa Kizayuni wa Israel, kuwa ndio waungaji mkono wakuu wa magaidi wanaotaka kuiangusha serikali halali ya Rais Bashar Assad na ambao hadi sasa wametenda jinai kubwa dhidi ya raia wa nchi hiyo.

No comments: