Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Hasira za walimwengu kwa utawala wa Kizayuni wa Israel

Hasira za walimwengu zinazoongezeka siku baada ya siku dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel zimezidi kuupotezea itibari utawala huo pandikizi licha ya kupita zaidi ya miongo sita ya kupandikizwa kwake katika kitovu cha ulimwengu wa Kiislamu na licha ya kutumiwa hila na uayari wa kila nui wa kuutafutia uhalali utawala huo dhalimu. Hivi sasa utawala wa Kizayuni unachukiwa zaidi duniani kuliko wakati mwingine wowote huku walimwengu wakidhihirisha hasira zao kwa utawala huo pandikizi kwa namna na njia mbalimbali. Wanaharakati wa kupigania amani kutoka nchi mbalimbali walioko katika Ukanda wa Ghaza wamefanya maandamano kulaani kuendelea kuzingirwa kidhulma ukanda huo na utawala ghasibu wa Kizayuni.
Waandamanaji hao wamewaenzi wanaharakati 9 wa kupigania amani waliouliwa katika msafara wa meli wa Marmara uliokuwa unaelekea Ukanda wa Ghaza kwenda kuvunja mzingiro wa ukanda huo. Mauaji hayo ya kikatili yalifanywa na makomandoo wa jeshi la Israel mwishoni mwa mwezi Mei 2010. Mwanaharakati wa amani kutoka Jordan, Kafah al Ma'ayira, ambaye ameshiriki katika maandamano hayo amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel haujali kufanya jinai yoyote ile katika njama zake za kujitanua hata kuua msafara wa watu wasio na silaha uliokuwa unaelekea Ghaza kwenda kuwasaidia binadamu wengine waliotumbukizwa kwenye mashaka makubwa na utawala wa Kizayuni wa Israel. Huko nchini Uhispania pia kumefanyika harakati ya jamii ya watu wa Vyuo Vikuu, kulaani jinai za Israel. Malalamiko hayo ya nchini Uhispania yalikuwa sehemu ya kampeni inayoungwa mkono na zaidi ya wasomi 350 wa Vyuo Vikuu vya nchi hiyo ya Ulaya wanaosisitiza kuwa taasisi za elimu za utawala wa Kizayuni zisusiwe na ziwekewe vikwazo kutokana na kushiriki katika kupanua teknolojia ya utawala huo ambayo inatumiwa kwenye vitendo vya kibaguzi. Sisitizo la kususiwa na kuwekewa vikwazo taasisi za kielimu za utawala wa Kizayuni limetolewa pia na vyama vya wanafunzi wa Vyuo Vikuu mbalimbali nchini Marekani. Miezi michache iliyopita Umoja wa Wanachuo wa Chuo Kikuu cha Wesleyan nchini Marekani ulipitisha azimio la kuzisusia taasisi za kielimu za Wazayuni kutokana na taasisi hizo kushiriki katika uvunjaji wa haki za binadamu katika ardhi za Palestina. Vyama mbalimbali vya wanachuo wa Vyuo Vikuu vya nchini Uingereza pia hivi karibuni vilitumia fursa ya mkutano wao wa kumaliza masomo kuwataka walimwengu waususie utawala wa Kizayuni wa Israel. Ususiaji na vikwazo vya vituo mbalimbali vya kielimu pamoja na Vyuo Vikuu na magazeti ya kona mbalimbali duniani dhidi ya utawala wa Kizayuni vimepata nguvu sana mwaka huu wa 2014. Matukio ya kimataifa yanaonesha kuwa, kutengwa utawala wa Kizayuni kimataifa hakuishii tu katika masuala ya kisiasa, kiuchimi na kidiplomasia, bali kutengwa Israel katika masuala ya kiutamaduni na Vyuo Vikuu nako kumeongezeka sana hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote. Jinai za utawala wa Kizayuni kwa wananchi wa Palestina zimezijeruhi vibaya nyoyo za walimwengu na jinai hizo ndizo zinazoongeza hasira za walimwengu dhidi ya Israel. Vile vile kuendelea siasa za utawala wa Kizayuni za kupora na kukalia kwa mabavu ardhi za Wapalestina na za mataifa mengine na kutokana na utawala huo kukaidi sheria zote za kimataifa kumezifanya nchi nyingi za dunia zikiwemo hata za barani Ulaya kushindwa kuvumilia na hivyo kuamua kuulalamikia utawala wa Kizayuni na kuchukua hatua za kivitendo vya kuwaunga mkono wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina na hususan wa Ukanda wa Ghaza, kwa lengo la kuwaondolea wakazi wa ukanda huo, mzingiro waliowekewa kila upande na Wazayuni kwa miaka kadhaa sasa.

No comments: