Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, May 21, 2014

Jenerali mstaafu wa Libya aungwa mkono na wanajeshi

Mkuu wa Vikosi vya Anga vya Libya ametangaza kuwa anamuunga mkono jenerali mstaafu Khalifa Haftar katika operesheni zake za kupambana na makundi yenye silaha katika mji wa Benghazi. Mkuu wa vikosi vya anga vya Libya pia amewataka wananchi kuuunga mkono jeshi la Haftar linaloitwa 'Jeshi la Taifa la Libya'. Haftar pia ameungwa mkono na Idara ya Upelelezi ya Kijeshi ya Libya.
Hayo yanajiri huku jeshi la Marekani likijitayarisha kuwaondoa raia wake katika ubalozi wa nchi hiyo mjini Tripoli na serikali ya mpito ya Libya kutangaza tarehe ya uchaguzi wa Bunge.
Machafuko yalishtadi Libya siku ya Ijumaa baada ya jenerali mstaafu Khalifa Haftar kuanzisha mashambulio ya anga na nchi kavu dhidi ya makundi ya wanamganbo katika mji wa Benghazi, ambayo baadhi yanaunga mkono serikali ya mpito ya Tripoli. Haftar ameapa kuwa hatoacha mashambulizi hayo hadi makundi yaliyofurutu ada yatakaposambaratika.

No comments: