Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 16, 2014

Marekani yatishia kuiwekea Russia vikwazo zaidi

Marekani imesema kuwa itaiadhibu Russia kwa kuiwekea vikwazo zaidi iwapo Moscow na washirika wake watavuruga uchaguzi ujao wa rais nchini Ukraine. John Kerry, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amesema katika mazungumzo na wenzake wa Ulaya kwamba, wananchi wa Ukraine wanapaswa kuachwa wajiamulie mustakbali wao na kwamba iwapo Russia au washirika wake watavuruga uchaguzi huo watawekewa vikwazo vya kiuchumi.

Serikali ya mpito ya Ukarine imepanga kufanya uchaguzi wa rais Mei 25 huku wasiwasi ukiongezeka katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo yanayotaka kujitenga.
Marekani na nchi za Ulaya zinaituhumu Russia kuwa inachochea machafuko nchini Ukraine hatua inayopelekea baadhi ya maeneo yatake kujitenga.

No comments: