Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

Morocco yawahukumu wanachama wa kundi la kitakfiri

Mahakama moja nchini Morocco imewahukumu kifungo jela wanachama 26 wa kundi moja la kitakfiri kwa tuhuma za kutuma wapiganaji katika sehemu mbalimbali za eneo la Sahel la Afrika kwa ajili ya kufanya mauji na vitendo vya kikatili. Mahakama hiyo imemuhukumu Mustapha Kadawi, kiongozi wa kundi hilo kifungo cha miaka 20 jela na kulipa faini ya kiasi cha Euro elfu 50. Mustapha anatajwa kuhusika katika kuunda na kuandaa mashambulizi ya kigaidi, kuunga mkono kifedha harakati za kigaidi, kuwashawishi wapiganaji wake kufanya vitendo hivyo, kuwa mwanachama wa kundi la kitakfiri lililopigwa marufuku nchini humo na kuitisha vikao mbalimbali bila kibali cha serikali.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo watu wengine 25 katika kesi hiyo wamehukumiwa vifungo vya miaka miwili hadi mitano na Mahakam hiyo. Morocco ilipiga marufuku ya makundi yenye misimamo ya kufurutu ada yapatayo 100, kufuatia miripuko ya mwaka jana katika mji wa Darul Baidha nchini humo. Hivi karibuni pia, serikali ya Rabat ilionyesha masikitiko yake kutokana na kuwepo baadhi ya harakati za kitakfiri zinazojihusisha na utumaji nchini Syria wapiganaji ambao baadaye hujiunga na makundi ya kigaidi kwa lengo la kutaka kuiangusha serikali halali ya Rais Bashar al-Assad wa nchi hiyo.

No comments: