Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

"Kupinduliwa serikali halali, chanzo cha matatizo"

Sergei Lavrov Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Russia amesema kuwa, migogoro mingi inayojitokeza katika nchi mbalimbali duniani husababishwa na juhudi za kutaka kuziondosha kimabavu na kinyume cha sheria serikali zilizoko madarakani. Lavrov ameongeza kuwa, migogoro yote iliyoshuhudiwa katika nchi za Syria, Libya, Iraq na hali kadhalika Ukraine, inatokana na kuwepo njama za kuzibadilisha serikali zilizoko madarakani kinyume cha sheria. Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Russia amesisitiza kuwa, kuna ulazima wa kuanzishwa mkakati wa kukomeshwa ukandamizaji na machafuko na kushirikisha makundi yote bila ya masharti yoyote.
Siku ya Jumatano iliyopita, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Russia alionya juu ya kutokea 'vita vya kindugu' nchini Ukraine. Lavrov alimtuhumu John Kerry Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani na viongozi wengine wa nchi za Ulaya kwa kusababisha mgogoro wa Ukraine. Lavrov amezitaka pande mbili zinazopigana nchini Ukraine kuketi kwenye meza ya mazungumzo ya amani, kwa lengo la kukomesha machafuko nchini humo.

No comments: