Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

Iran kuwa mwenyeji wa kikao cha marafiki wa Syria

Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, jiji la Tehran kuanzia kesho litakuwa mwenyeji wa kikao cha pili cha Wakuu wa Kamisheni za Usalama wa Taifa kutoka nchi marafiki wa Syria. Alauddin Bourujerdi ameongeza kuwa, wajumbe kutoka nchi zisizopungua 25 watashiriki kwenye kikao hicho. Bourujerdi ameongeza kuwa, vikao hivyo vinafanyika kwa shabaha ya kusaidia kukomesha mapigano nchini Syria sanjari na kuyapa nguvu mapambano ya muqawama dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni wa Iran amesisitiza kwamba kuna ulazima wa kuendelezwa zoezi la upelekaji misaada ya kibinadamu kwa wananchi wa Syria ikiwemo chakula na madawa. 

No comments: