Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

Riek Machar: Tunataka amani irejee Sudan Kusini

Kiongozi wa waasi wa Sudan Kusini na Makamu wa zamani wa Rais wa nchi hiyo Riek Machar amesema ana nia ya kweli ya kutaka amani na yuko tayari kuendelea na mazungumzo juu ya suala hilo. Katika taarifa aliyotoa mjini Nairobi, Kenya hapo jana, kufuatia mazungumzo yake na Rais Uhuru Kenyatta wa nchi hiyo, Machar amesema na hapa ninamnukuu:"Nimekuja kusukuma mbele mchakato huu; na ninataka nikuhakikishieni kwamba tuna nia ya dhati kuhusu kuleta amani Sudan Kusini", mwisho wa kumnukuu.
Duru ijayo ya mazungumzo kati ya serikali ya Sudan Kusini na waasi wanaopigana na jeshi la serikali hiyo imepangwa kufanyika tarehe 4 ya mwezi ujao wa Juni huko mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Wakati huohuo imeelezwa kuwa Jumuiya ya Kieneo ya nchi za Afrika Mashariki IGAD itatuma kikosi cha kusimamia makubaliano ya usitishaji vita huko Sudan Kusini. Mwakilishi wa IGAD nchiniSudan Kusini Jenerali Lazaro Sumbeiywo amesema kikosi hicho kitatumwa nchini humo mwezi ujao wa Juni kwa madhumuni ya kusimamia utekelezaji mzuri wa makubaliano ya usitishaji mapigano kati ya vikosi vya serikali na vile vya waasi. Amesema nchi zinazotarajiwa i kuchangia askari wa kikosi hicho ni Ethiopia, Djibouti, Kenya, Rwanda na Burundi

No comments: