Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

Mahama: Hatutoingojea UN kukabiliana na migogoro

Rais John Dramani Mahama wa Ghana amesema Jumuiya ya Uchumi ya Nchi za Magharibi mwa Afrika ECOWAS itatekeleza jukumu lake kuhusiana na migogoro katika nchi za Nigeria na Mali. Rais wa Ghana amesisitiza kwamba nchi za Magharibi mwa Afrika hazitoruhusu maendeleo yaliyoletwa na wananchi wa nchi hizo yavurugwe kutokana na hatua za ubinafsi za baadhi ya makundi.
Akizungumza baada ya kikao cha dharura cha ECOWAS kilichofanyika jana usiku katika mji mkuu wa Ghana Accra, Dramani Mahana ambaye ni mwenyekiti wa sasa wa jumuiya hiyo amesema nchi wanachama wa ECOWAS hazitoungojea Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kukabiliana na kupambana na migogoro na machafuko. Rais wa Ghana amebainisha kuwa nchi za Kiafrika zinakabiliwa na aina mpya ya vitisho na kwamba tishio dhidi ya nchi yoyote ya bara hilo linahesabiwa kuwa tishio kwa nchi zote za Magharibi mwa Afrika. Hali si shwari nchini Nigeria baada ya wanafunzi wa kike zaidi ya 200 wa shule ya Chibok iliyoko katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa nchi hiyo kutekwa nyara na kundi la Boko Haram mwezi uliopita wa Aprili. Huko kaskazini mwa Mali pia kunashuhudiwa wimbi jipya la machafuko lililoanzishwa na wapinzani wa serikali

No comments: