Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Iran iko tayari kuisaidia Nigeria kukomboa wanafunzi

Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran anayeshughulikia masuala ya nchi za Kiarabu na Kiafrika amesema kuwa, Tehran iko tayari kuisaidia Nigeria katika kuipatia ufumbuzi kadhia ya kutekwa nyara wanafunzi wa kike zaidi ya 200. Hossein Amir-Abdollahian amesema hayo katika mazungumzo yake na Tukur Mani, balozi wa Nigeria hapa mjini Tehran na kusisitiza kwamba, serikali ya Iran inatangaza utayarifu wake wa kuisaidia Nigeria katika kuwakomboa wasichana hao wanaoshikiliwa na kundi la Kitakfiri la Boko Haram.
Kwa upande wake Tukur Mani, balozi wa Nigeria hapa mjini Tehran ameishukuru serikali ya Iran kwa kuwa pamoja na serikali na taifa la Nigeria sambamba na hatua ya Tehran ya kulaani vitendo vya kigaidi. Wakati huo huo, Hamid Reza Dehqani, Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC amezitaka nchi za Kiislamu kukabiliana na makundi ya kitakfiri kama lile la Boko Haram la nchini Nigeria. Wanafunzi hao wa kike walitekwa nyara na kundi la Boko Haram tarehe 14 ya mwezi uliopita katika shule moja ya sekondari iliyoko katika mji wa Chobok kwenye jimbo la Borno.

No comments: