Kuendelea kuvurunda serikali ya Marekani
katika masuala mbalimbali ya kimataifa kumewafanya wadau mbalimbali
wakiwemo wanasiasa wa nchi hiyo kuingiwa na wasiwasi kuhusu mustakabali
wa kisiasa, kijeshi na kiuchumi wa nchi yao. Gavana wa jimbo la New
Jersey, Chris Christie amenukuliwa akisema kuwa, Marekani imepoteza
ushawishi wake na kwa sasa nchi hiyo haiko kwenye nafasi ya kwanza
katika orodha ya nchi zenye satua na nguvu kubwa duniani. Gavana wa New
Jersey anailaumu serikali ya Rais Barack Obama na sera zake za nje
akisema ikulu ya White House imepoteza dira na kwa mantiki hiyo,
mustakabali wa Marekani kimataifa unakumbwa na atiati.
Kuna uwezekano
mkubwa Chris Christie akawania urais kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka
2016 kwa tiketi ya chama cha Republicans. Mwanasiasa huyo anasema zama
za Rais Ronald Regan Marekani ilikuwa na nguvu na satua katika kila
nyanja na kwamba iliweza kuainisha marafiki na maadui zake lakini satua
hiyo imefifia na inakabiliwa na hatari ya kutoweka katika siku za usoni.
Matamshi ya Gavana wa New Jersey
yanahesabiwa kuwa sehemu ya mashindano ya kisiasa kati ya vyama vya
Republicans na Democrats kabla ya uchaguzi mkuu ujao. Kwa mtazamo wa
chama cha upinzani cha Republicans na pia idadi kubwa ya wadau na
wafuasi wa chama tawala cha Democrats ni kwamba, kuanzia muongo wa 50
hadi 80, Marekani ilikuwa na uwezo mkubwa na kwa mahesabu ya haraka
Washington ilikuwa ikitawala zaidi ya asilimia 50 ya dunia. Wakati huo
viongozi wa Marekani walifanya chochote walichokitaka kwa njia ya moja
kwa moja au kupitia waitifaki wao bila matatizo yoyote. Marekani kupitia
njia hiyo iliweza kuwashinikiza viongozi mbalimbali waliokuwa wakipinga
mfumo wake wa kibeberu na pale mashinikizo yalipoonekana kutozaa
matunga basi Washington iliweza kuwapindua na kuwaondoa madarakani
viongozi hao kwa kutumia nguvu za kijeshi za moja kwa moja au kupitia
waitifaki wake.
Kwa sasa mambo yamebadilika na hali hiyo
haipo tena. Mambo mengi yamepelekea kudhoofika satua ya Marekani
kimataifa hususan katika kipindi cha utawala wa George W. Bush wa chama
cha Republicans na Rais Barack Obama kutoka Democrats. Wachambuzi wengi
wanaamini kuwa, matukio ya miaka ya hivi karibuni kama vile uvamizi wa
Marekani nchini Iraq kinyume na sheria za kimataifa, ujasusi wa
kupindukia wa Washington dhidi ya nchi na viongozi mbalimbali wa dunia
hata wale wanaodaiwa kuwa ni waitifaki wake, ukiukaji mkubwa wa haki za
binadamu wa Marekani katika jela za Abu Ghureib na Guantanamo ni
miongoni mwa mambo yanayoifanya nchi hiyo kupoteza umashuhuri kwa kasi
ya ajabu.
Tangu mwishoni mwa karne ya 20 dalili za
kuporomoka satua ya Marekani kimataifa zilikua zimeanza kuonekana na
hata baadhi ya weledi wa mambo wakatabiri kwamba Washington itapoteza
uwezo wake wa kiuchumi na kijeshi duniani kwa mataifa kama vile China na
Japan. Utabiri huo unaelekea kutimia kwani kwa sasa nchi hiyo
inakabiliwa na madeni chungu nzima na takwimu zinaonyesha kuwa madeni
hayo yamepindukia dola trilioni 17
No comments:
Post a Comment