Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 17, 2014

Galloway: El Sisi ni mbaya zaidi kuliko Mubarak

George Galloway, mbunge mashuhuri wa bunge la Uingereza amesema Abdel Fattah el Sisi, mgombea urais wa Misri ni mbaya zaidi kuliko Hosni Mubarak, dikteta wa nchi hiyo aliyeng’olewa madarakani. Akihutubia jamii ya Wamisri waishio nchini Austria katika kongamano lililofanyika kwa anuani isemayo:”Watetezi wa uhuru duniani wako dhidi ya mapinduzi ya kijeshi”, Galloway amesema harakati za kimapinduzi nchini Misri zitaushinda ufisadi ndani ya nchi hiyo akiwemo mgombea wa kiti cha urais Abdel Fattah el Sisi.
Mbunge huyo wa Uingereza amesema, el Sisi ni dikteta na kufafanua kwamba Abdel Fattah el Sisi ni mbaya zaidi kuliko Hosni Mubarak, dikteta wa Misri aliyeng’olewa madarakani na anaungwa mkono na Marekani na kupewa msukumo kwa utajiri wa baadhi ya nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi. Galloway amemueleza el Sisi kuwa ni mabaki ya utawala wa Mubarak na kutangaza uungaji mkono wake kwa wanamapinduzi wote wa Misri katika mapambano dhidi ya el Sisi. Mbunge huyo wa Uingereza aidha amesema tuhuma za mashtaka dhidi ya Muhammad Morsi, rais wa Misri aliyeng’olewa madarakani ni za uwongo na hazina ukweli na akalaani pia hatua ya kuitangaza harakati ya Ikhwanul Muslimin kuwa ni kundi la kigaidi

No comments: